Kwa nini hatukuuona ushindi wa Lissu?

  Na Ezekiel Kamwaga     AKIANDIKA mapitio ya kitabu cha The Age of Revolutions cha Fareed Zakaria kwenye jarida mashuhuri la Foreign Policy Machi mwaka jana, mchambuzi Michael Hirsh, aliandika mstari mmoja ambao umebaki kwenye kumbukumbu zangu; “Kuna kitu kimeikumba dunia hivi sasa na sote bado hatujajua ni kitu gani”.     Hayo yalikuwa […]

Kazini kwao kuna kazi

  Na Ezekiel Kamwaga     UTANGULIZI     WAKATI mwaka mpya unapoanza, vyombo vya habari vimekuwa na utamaduni wa kufanya tafakuri kuhusu masuala tofauti yaliyotokea katika mwaka uliokwisha na yapi ya kutarajia katika mwaka mpya.     Kwa mara ya kwanza mwaka huu, Gazeti la Dunia linafanya uchambuzi wa kuangalia wanasiasa wa kuangaliwa zaidi […]

Kosa la Freeman Mbowe

  Na Ezekiel Kamwaga     MWAKA 2015, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilipata mafanikio makubwa katika Uchaguzi Mkuu wa Tanzania. Kilipata takribani asilimia 40 ya kura zote zilizopigwa – kiwango ambacho kilikuwa hakijawahi kufikiwa na chama chochote cha upinzani katika historia ya taifa letu.     Kulikuwa na mambo mawili katika ushindi huo […]

Kosa la Tundu Lissu

Picha kwa Hisani ya Gazeti la Citizen la Tanzania   Na Ezekiel Kamwaga   MARA nyingi ninapofanya uchambuzi kuhusu wanasiasa, huwa ninaamini kuwa kuna wanasiasa wa aina tatu; wanasiasa wa kipekee, wanasiasa wa kitaasisi na wanasiasa wa msimu.   Wanasiasa wa kipekee ni wale ambao si wa kawaida. Nazungumzia watu wa aina ya Nelson Mandela […]

Ancien Regime, Abdul Nondo na watu kutekwa

  Na Ezekiel Kamwaga     KATIKA uchambuzi wake wa nini kilisababisha Mapinduzi ya Ufaransa ya mwaka 1789, Alexis du Tocqueville aliandika kitu cha tofauti na wengine walioandika kuhusu mapinduzi yale. Alisema mapinduzi yale hayakuwa tukio la mara moja bali ni hitimisho la miaka mingi ya kuharibika kwa mfumo wa utawala wa taifa hilo.   […]

Rais Samia wa G20

MAELEZO YA PICHA: Rais Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo ya uwili (bilateral)  na Rais wa Indonesia, Prabowo Subianto, pembezoni mwa mkutano wa G20 uliofanyika Rio de Janeiro, Brazil, wiki iliyopita.   Na Ezekiel Kamwaga   MOJAWAPO ya taswira zilizobaki kwenye kumbukumbu zangu kuhusu Mkutano wa Nchi Tajiri Duniani maarufu kwa jina la G20 uliomalizika […]

Ajali ya Kariakoo, angani na Rio: Saa 15 za kwanza

  Na Ezekiel Kamwaga   DAKIKA chache baada ya ndege iliyombeba Rais Samia Suluhu Hassan kupaa angani kwenda Brazil kuhudhuria mkutano aliopewa heshima ya kualikwa wa Nchi Tajiri Duniani wa G20, habari zilianza kusambaa mitandaoni kuhusu kuanguka kwa jengo la biashara katika eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam.   Kwa bahati nzuri, ndani ya […]

Septemba 23 isiwe maafa, uwe mwanzo mpya

  Na Ezekiel Kamwaga   KESHO, Septemba 23, 2024, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepanga kufanya maandamano hapa nchini kupinga vitendo vya utekaji na mauaji vinavyoonekana kukithiri hapa nchini hivi sasa.   Mpaka wakati naandika makala haya, ninafahamu kwamba CHADEMA wameamua kesho watafanya maandamano hayo. Na mpaka wakati huu, Polisi hawajatoa taarifa yoyote kuruhusu […]

Chawa ni nani?

Tajiri Elon Musk wa Marekani (kushoto) katika picha na mgombea urais wa chama cha Republican, Donald Trump. Picha kwa hisani ya IBTimesUK     Na Ezekiel Kamwaga     KWA wafuatiliaji wa siasa za Marekani kuelekea uchaguzi wao wa Novemba mwaka huu, watakuwa wamebaini namna Elon Musk; mmoja wa matajiri wakubwa duniani, anavyomuunga mkono mgombea […]

Babu Duni na binti yangu: Somo la Unyenyekevu  

  Na Ezekiel Kamwaga   SIKU moja majira ya saa tano usiku, nilipokea simu kutoka kwa mwanasiasa mkongwe wa Zanzibar, Juma Duni Haji. Alikuwa ananipigia kwa vile hakupokea wakati alipopigiwa simu kutoka kwangu saa kadhaa nyuma.   Nilipoiona tu nilitabasamu maana nilijua kilichotokea. Sikuwa nimempigia mimi isipokuwa binti yangu mwenye umri wa miaka mitatu wakati […]