Tunafuturu futari, hatufutari futuru

  Na Ahmed Rajab   MIAKA kadhaa iliyopita katika siku kama hizi za mfungo wa Ramadhani niliwahi kuandika makala katika gazeti la Raia Mwema ambamo nililalama jinsi aina kwa aina ya mapishi asilia ya Kiswahili yalivyotoweka Zanzibar baada ya Mapinduzi ya 1964.     Nilijawa na furaha nilipoona kwamba makala hayo yaliwachochea wengine kuendeleza na […]

Senegal: Funzo kubwa zaidi ni wapinzani kuaminiana

Rais Macky Sall wa Senegal akiwatembeza Rais mteule wa Senegal, Diomaye Faye (kushoto kwake) na Ousmane Sonko (kulia kwake)  kwenye Ikulu ya Dakar hivi karibuni. Picha kutoka mtandao wa Quest France.   Na Zitto Kabwe   Mtandao wa Viongozi wa Upinzani katika Bara la Afrika (Pan African Opposition Leaders Solidarity Network) umepoteza wanachama wake wawili […]

“Sit down and talk”: Uchambuzi wangu

Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Karume (kushoto) katika mojawapo ya mazungumzo ya faragha aliyowahi kuyafanya na aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, marehemu Seif Shariff Hamad, kisiwani Unguja. Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi.   Na Ezekiel Kamwaga   BAADA ya maneno ya kujibizana baina ya viongozi wa vyama viwili vikuu vya siasa visiwani Zanzibar […]

KC Dorothy Semu: Kupanda, sababu na changamoto  

  Ezekiel Kamwaga   MIAKA michache iliyopita, Dorothy Semu – wakati huo akiwa Katibu Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, alianza kupokea simu; za kushawishi na kumtisha, kutaka akihame chama chake na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakati wa wimbi kubwa lililokuja kufahamika baadaye kama “kuunga mkono juhudi”.   Waliokuwa wakiwasiliana naye, walimuahidi vyeo […]

IWD: Ushiriki wa siasa usisubiri nyakati za uchaguzi pekee

Na Fortunata Kitokesya   SIKU ya Kimataifa ya Wanawake Duniani (International Women’s Day) ina mchango mkubwa kwa usawa na haki za wanawake wote duniani. Ni siku muhimu ya kutambua mapambano endelevu ya usawa wa kijinsia na kusherehekea mafanikio ya wanawake ulimwenguni kote.   Pia ni siku ambapo watu binafsi, mashirika, na jamii wanakusanyika kwa pamoja […]

TAABINI YA MZEE ALI HASSAN MWINYI

TAABINI Ali Hassan Mwinyi “Mzee Rukhsa”: (Mei 8,1925 – Februari 29, 2024) Mtu wa watu aliyependwa na masharifu ALHAJI Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki dunia Dar es Salaam, Alhamisi iliyopita, siku 70 kabla ya kutimia miaka 99, aliushangaza ulimwengu alipoibuka kuwa Rais wa tatu wa Zanzibar 1984. Mwinyi aliushangaza tena ulimwengu miezi kadhaa baadaye alipochomoza kuwa […]

Kupotea: Kazi ya kwanza ya dola ni kutulinda

Na Ezekiel Kamwaga KABLA ya kuandika kile nilichotaka kuandika, ni muhimu sana kuweka msingi. Na msingi wenyewe, kwa kukosa mifano ya karibuni sana, itabidi nirudi nyuma takribani miaka 365.  Mwaka 1659, kitabu cha Leviathan cha Thomas Hobbes kilichapwa kwa mara ya kwanza. Hoja yake kubwa ilikuwa kwamba wananchi wanatakiwa kuipa dola nguvu isiyo ya kawaida […]

Afrika Kusini ilicheza na shingo ilitoa

Picha: Mmoja wa waandamanaji akifurahia hukumu ya Mahakama ya Haki ya Kimataifa (ICJ) dhidi ya Israel jijini The Hague hivi karibuni. Picha kwa hisani ya Foreign Policy   Na Ahmed Rajab   ISRAEL haina uso.  Inajaribu kujikaza kisabuni na kujitoa kimasomaso lakini Mahakama ya Kimataifa (ICJ), mjini Hague, Uholanzi, yameiumbua kwa unyama inaoufanya dhidi ya […]

Kamari ya Rais Samia kwa Nchimbi

Picha: Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan akiteta na Katibu Mkuu mpya wa chama hicho, Emmanuel Nchimbi, mara baada ya kupewa majukumu hayo mjini Zanzibar wiki hii. Picha kwa hisani ya CCM.    Na Ezekiel Kamwaga   KUCHAGULIWA kwa Dk. Emmanuel Nchimbi kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumeibua swali moja […]

Afrika katika mkorogo wa vita vya Gaza

Rais Joe Biden akiwa na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu. Picha ya Shirika la AP   Na Ahmed Rajab   ZAIDI ya siku mia zimekwishapita tangu majeshi ya Israel yaanze kulitwanga eneo zima la Ukanda wa Gaza, ikiwa ni hatua ya kulipiza kisasi mashambulio yakushangaza dhidi ya Israel yaliyofanywa na Mvuvumko wa Muqawama wa […]