Nani atataka kuwa Katibu Mkuu wa CCM?

Picha: Daniel Godfrey Chongolo. Kwa hisani ya tovuti ya CCM.   Na Ezekiel Kamwaga   WIKI mbili zilizopita, mmoja wa rafiki zangu ambaye ni kiongozi serikalini, alikuja Dar es Salaam kikazi. Katika mazungumzo yetu tulipoonana, suala la kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, lilichukua sehemu kubwa ya mazungumzo yetu.   […]

Mafunzo kutoka Zambia

  Na Ezekiel Kamwaga   OKTOBA mwaka huu, nilikuwa sehemu ya waandishi wa habari wa Tanzania waliokuwa kwenye ziara ya kitaifa ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Zambia. Ingawa vyombo vyetu vya habari viliandika kuhusu masuala makubwa yaliyotokea huko, jicho langu lilivutwa na jambo lingine dogo nililoshuhudia.   Oktoba 24, nilipata fursa ya kuhudhuria sherehe […]

Wakati Kissinger alivyomlazia Nyerere

Rais Julius Nyerere akiwa na Henry Kissinger jijini Dar es Salaam mwaka 1976. Picha kwa Hisani ya Cambridge University Press   Na Ahmed Rajab   DAKTA Henry Kissinger aliyefariki dunia Kent, Connecticut, Marekani, Novemba 29 mwaka huu alikuwa mwingi wa mengi.  Alikuwa msomi wa hali ya juu, gwiji wa diplomasia, mshauri wa siasa za kimataifa […]

Waisraeli wanaiogopa hata furaha ya Wapalestina

Picha kwa Hisani ya Pars Today Na Ahmed Rajab KISWAHILI chetu hakina neno moja lenye tafsiri ya neno la Kiingereza ‘resistance.’ Lakini lugha za Kiarabu na Kifarsi (Kiajemi), ambazo tumezoea kuazima misamiati yao, zote zinalo neno moja lenye maana ya ‘resistance.’ Na lugha zote hizo mbili zinalitumia neno hilo hilo moja lililoanzia kwenye Kiarabu: ‘muqawama.’ […]

Katibu Mkuu wa CCM: Historia Fupi

Na Ezekiel Kamwaga DANIEL Godfrey Chongolo amemaliza muhula wake kama Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuandika barua ya kujiuzulu na kuhitimisha takribani miaka miwili na miezi saba ya kutumikia nafasi hiyo. Wakati alipotangazwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, si watu wengi walikuwa wamewahi kumsikia kabla – ingawa aliwahi kuwa Mkuu wa […]

Joan Wicken, mwanamke aliyemjua Julius Nyerere

Picha: Nakala ya kitabu kilichoandikwa na Profesa Aili Mari Tripp kuhusu maisha ya Joan Wicken na uhusiano wake na Mwalimu Nyerere. Kitabu hicho kimechapwa na kampuni ya Mkuki na Nyota   Na Ahmed Rajab   KWA zaidi ya miaka 40, kila alasiri baada ya saa za kazi, Bi Joan Wicken alikuwa akikimbilia Msasani, Dar es […]

Maji kila sehemu lakini hakuna maji!

Na Ezekiel Kamwaga   “Maji kila mahali lakini hakuna hata tone moja la kunywa” Samuel Taylor Coleridge, The Rime of the Ancient Mariner   MWANZO kabisa, napenda kutoa pole kwa Watanzania wenzangu ambao wameathirika kwa namna moja au nyingine na mvua hizi za El Nino zinazoendelea kunyesha.   Ninafanya kazi kwenye kituo cha televisheni na […]

Fungulia John Heche Suguta

Picha: John Heche (kwa hisani ya mtandao wa Millard Ayo)   Na Ezekiel Kamwaga   MWAKA 2016 utabaki kuwa na historia ya kipekee kwenye miaka ya karibuni na pengine mingi inayokuja. Huu ndiyo mwaka ambapo neno moja lilitajwa kuwa neno lililotumika zaidi katika lugha za Kijerumani na Kihispania mtawalia; Postfaktisch na Posverdad. Kwenye Kiingereza, linajulikana […]

Bahati na kupanda kwa Dk. Tulia Ackson

Picha: Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) akizungumza baada ya kupokewa katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma mara baada ya kurejea nchini akitokea nchini Angola alikoshinda uchaguzi wa taasisi hiyo ya mabunge duniani. Picha kwa hisani ya mtandao wa Zanzinews.   Na Ezekiel Kamwaga   WAKATI Ikulu ilipotoa […]

Taabini: Hashil Seif, mpigania haki asiyeyumba (Januari 12, 1938 – Oktoba 27, 2023)  

  Na Ahmed Rajab   UJUMBE wa simu ulipoingia asubuhi ya Ijumaa iliyopita, ulikuwa na maneno machache: “Ndugu yetu ameshatangulia mbele ya Haq leo saa moja na dakika arobaini na tano kwa saa za hapa. Tunangoja daktari aje kumtizama mara ya mwisho.”   Aliyeleta ujumbe alikuwa Hamed Hilal, mmoja wa makomredi wa chama cha zamani […]