Ni nani makomredi walioshiriki Mapinduzi ya Zanzibar 1964?

Picha: Baraza la Kwanza la Mapinduzi Zanzibar WIKI iliyopita mwandishi Salma Said alichangia katika mazungumzo ya humu mtandaoni yaliyoanzishwa na makala ya @ahmedrajab katika Gazeti la Dunia yakimzungumzia Badawi Qullatein.    Salma aliandika kuwa yeye aliwahi kukutana na kuzungumza na Badawi.  Akawataja pia makomredi wakuu wengine wa Umma Party aliowahi kukutana nao, kwa mfano Ali […]

Muungano @59: Israel ilihusika mwaka 1964?

Picha: Marais Julius Nyerere wa Tanganyika na Abeid Amani Karume wakitia saini Hati za Muungano. Na Ezekiel Kamwaga MARA ya kwanza kusikia jina la Misha Feinsilber ilikuwa wakati niliposoma – kwa mara ya kwanza pia, kitabu adhimu cha Harith Ghassany “Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru (2010) ” takribani muongo mmoja uliopita. Mara ya pili ikawa kwenye […]

Namna ya kukabili hoja za dunia mpya anayoitaka Rais XI Jinping

Picha ya Xi: Kwa hisani ya AP/Andy Wong.  Na Mark Leonard KATIKA siku za karibuni, Rais Xi Jinping wa China ametawala vichwa vya habari katika vyombo vya Magharibi kwa matukio makubwa mawili. Mosi ni kwa namna alivyofanikisha mazungumzo baina ya Iran na Saudi Arabia na pili ziara yake nchini Russia ambako alitoa mawazo yake kuhusu […]

Kwa nini Dk. Mpango hawezi kupoa (2)?

Na Ezekiel Kamwaga KATIKA sehemu ya kwanza ya makala haya wiki iliyopita, nilitaka kuweka historia kidogo ya nafasi ya Makamu wa Rais tangu mwaka 1995. Hii ni kwa sababu, Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995 ndiyo ulikuwa wa kwanza ambapo nafasi ya mgombea mwenza (Makamu wa Rais) ilikuwepo.   Kabla ya mwaka 1995 – yaani kuanzia […]

Mara hii nina hofu na Sudan

Picha kwa hisani ya mtandao wa Africanintelligence.  MACHAFUKO yameanza upya nchini Sudan. Mgogoro wa sasa ni mbaya kwa sababu unahusisha watu wawili wenye silaha – Mkuu wa Majeshi, Jenerali Abdel Fatah al Burhan na Kiongozi wa Vikosi vya Mgambo, Jenerali Mohamed Hamdani Dagalo maarufu kwa jina la Hemedti. Kwangu, huu unaweza kugeuka kuwa mgogoro mbaya […]

Kwa nini Dk. Mpango hawezi kupoa?

 Picha kwa Hisani ya gazeti la serikali la Daily News. KITABIA, nafasi ya Makamu wa Rais katika nchi inayofuata mfumo wa uchaguzi wa Kimarekani – kama ilivyo kwa sehemu hapa kwetu Tanzania, ni nafasi iliyopoa na inayoboa. Enzi nikiwa ripota, mara mbili niliwahi kutumwa na mhariri wangu kwenda kuandika kuhusu mkutano wa mmoja wa Makamu […]

Mzigo wa Rais Samia, Mbowe na Zitto

Na Ezekiel Kamwaga KUTOKANA na kuimarika kwa mahusiano ya kisiasa baina ya vyama vitatu vikubwa vya siasa nchini Tanzania; Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ACT Wazalendo, maswali yameibuka – nani anapata nini kwenye maridhiano haya ya kisiasa? Ninawafahamu wanasiasa wawili wabunge wa CCM ambao wamezungumza nami wakionesha wasiwasi mkubwa […]

Msuya: Waambieni wananchi ukweli

   WAZIRI Mkuu mstaafu, Cleopa David Msuya (92), ametoa siri ya namna ya kudumu madarakani na Watanzania pasipo migogoro; kuwaeleza ukweli. Katika mazungumzo yake na Gazeti la Dunia, Msuya alisema jambo kubwa alilojifunza kwenye utumishi wake wa umma uliodumu kwa takribani nusu karne, ni kwamba kama watu wakiambiwa ukweli na kuelewa, viongozi hawatakuwa na kitu […]

Pumba na mchele kwenye maandamano ya Kenya

Na Willy Mutunga IBARA ya 37 ya Katiba ya Kenya inampa Raila Odinga na Wakenya wengine haki ya kuandamana, kufanya kusanyiko na kufanya shinikizo kwa njia ya amani, bila vurugu au kubeba silaha.   Kwenye mazingira ya namna hii, wajibu wa kikatiba wa vyombo vya dola wakati wa maandamano ni kuhakikisha kuwa haki hiyo ya […]

Lowassa apigania uhai Afrika Kusini

HALI ya kiafya ya Waziri Mkuu mstaafu, Edward Ngoyai Lowassa, inaelezwa kuwa ya kutoridhisha katika siku za karibuni na kwamba sasa “anapigania uhai wake”, Gazeti la Dunia linaweza kuthibitisha. Lowassa anayetarajiwa kutimiza umri wa miaka 70 Agosti 26 mwaka huu, amelazwa nchini Afrika Kusini alikopelekwa mwanzoni mwa mwaka jana kwa matibabu zaidi baada ya awali […]