Kujenga au kubomoa si usanii, ni siasa

  Na Ezekiel Kamwaga   KUNA uhusiano wowote kati ya siasa na majengo? Kuna uhusiano wowote baina ya viongozi na matukio ya kujenga au kubomoa vitu? Jibu langu ni ndiyo na makala yangu hii itaeleza juu ya mifano na namna kujenga au kubomoa kunavyoweza kumjenga mwanasiasa au utawala mbele ya wananchi wake.   Ninaandika makala […]

“Sit down and talk”: Uchambuzi wangu

Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Karume (kushoto) katika mojawapo ya mazungumzo ya faragha aliyowahi kuyafanya na aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, marehemu Seif Shariff Hamad, kisiwani Unguja. Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi.   Na Ezekiel Kamwaga   BAADA ya maneno ya kujibizana baina ya viongozi wa vyama viwili vikuu vya siasa visiwani Zanzibar […]

KC Dorothy Semu: Kupanda, sababu na changamoto  

  Ezekiel Kamwaga   MIAKA michache iliyopita, Dorothy Semu – wakati huo akiwa Katibu Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, alianza kupokea simu; za kushawishi na kumtisha, kutaka akihame chama chake na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakati wa wimbi kubwa lililokuja kufahamika baadaye kama “kuunga mkono juhudi”.   Waliokuwa wakiwasiliana naye, walimuahidi vyeo […]

Kupotea: Kazi ya kwanza ya dola ni kutulinda

Na Ezekiel Kamwaga KABLA ya kuandika kile nilichotaka kuandika, ni muhimu sana kuweka msingi. Na msingi wenyewe, kwa kukosa mifano ya karibuni sana, itabidi nirudi nyuma takribani miaka 365.  Mwaka 1659, kitabu cha Leviathan cha Thomas Hobbes kilichapwa kwa mara ya kwanza. Hoja yake kubwa ilikuwa kwamba wananchi wanatakiwa kuipa dola nguvu isiyo ya kawaida […]

Kamari ya Rais Samia kwa Nchimbi

Picha: Mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan akiteta na Katibu Mkuu mpya wa chama hicho, Emmanuel Nchimbi, mara baada ya kupewa majukumu hayo mjini Zanzibar wiki hii. Picha kwa hisani ya CCM.    Na Ezekiel Kamwaga   KUCHAGULIWA kwa Dk. Emmanuel Nchimbi kuwa Katibu Mkuu mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumeibua swali moja […]

Mtihani wa Rais Samia na Waziri Ummy

Na Ezekiel Kamwaga   MWISHONI mwa wiki hii, nilikuwa na mjadala mzuri katika mojawapo ya makundi sogozi niliyopo. Rafiki yangu mmoja alijenga hoja kwamba tatizo la akinamama kujifungulia sakafuni lililotawala sana katika vyombo vya habari na mitandaoni hapa nchini au mwenendo wa suala la Naibu Waziri wa zamani wa Sheria na Katiba, Pauline Gekul, yasingetokea […]

Lamata: Taa ya Tamthilia za Nyumbani

Na Ezekiel Kamwaga MWAKA 2017 alijitambulisha kupitia tamthilia ya Kapuni iliyorushwa na kituo cha DSTV. Tangu wakati huo, Leah Richard Mwendamseke, amekuwa akifyatua tamthilia ambazo zimekuwa sehemu ya maisha ya Watanzania – sasa akitamba na ile ya Jua Kali. Kwa wengi, Mwendamseke ni alama ya tamthilia za Kitanzania na safari yake haikuwa rahisi. Yeye ni […]

Teri: Tanzania ya Uwekezaji

Na Ezekiel Kamwaga NAMBA zinazungumza kuliko maneno. Mwanzoni mwa mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan, alimteua Gilead Teri, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Wakati anapewa nafasi hiyo, wastani wa miradi ya uwekezaji iliyokuwa inarekodiwa na kituo hicho kwa miaka mitatu ya nyuma ilikuwa takribani 56. Katika mwaka wake wa kwanza tu, […]

Mkenda: Mageuzi ya Elimu

Na Ezekiel Kamwaga INGAWA kitaaluma ni mchumi, Profesa Adolf Mkenda, amejipambanua katika mwaka huu kama mwanasiasa anayetaka kuona mabadiliko kwenye sekta ya elimu ili iendane na changamoto za kisasa nchini na kimataifa. Kuanzia mwakani, Wizara ya Elimu imeandaa mitaala mipya ambayo itawafanya wahitimu kuwa na maarifa zaidi na uwezo mkubwa zaidi wa kukabili changamoto za […]

Karia: Rais wa Mpira

Na Ezekiel Kamwaga MWAKA 2023 umeshuhudia Tanzania ikipewa nafasi ya kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yaliyopangwa kufanyika mnamo mwaka 2027. Tanzania itaandaa mashindano hayo kwa ushirikiano wa pamoja kati yake na jirani zake wa Kenya na Uganda. Hata hivyo, hakuna shaka kwamba Tanzania ndiyo hasa ilifanikisha ushindi […]