January: Alama kila anapoenda

Na Ezekiel Kamwaga MFANO mmoja unatosha kumueleza Waziri wa Mambo ya Nje, January Makamba, na utendaji wake tangu alipoingia kwenye wizara hiyo mwaka huu. Kwenye ndege wakati tukirejea Dar es Salaam kutoka India kwenye ziara ya kitaifa ya Rais Samia nchini humo, mmoja wa mawaziri alinieleza kwamba tangu awe waziri – ziara ile ilikuwa ndiyo […]

Zitto: Kaka wa Maridhiano

Na Ezekiel Kamwaga MWANZONI mwa mwaka huu, Kiongozi wa Chama wa  ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, alikuwa pengine mwanasiasa aliyekuwa akishambuliwa zaidi mitandaoni kuliko mwingine. Mashambulizi hayo yalitokana na ushiriki wake katika Kikosi Kazi kilichoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mapitio ya sheria za uchaguzi zilizopo nchini. Kikosi kazi hicho hakikuwa kinaungwa mkono na chama […]

Hussein Bashe: Kilimo ni dili

Na Ezekiel Kamwaga SIKU moja tukiwa New Delhi, India, kwenye ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, alifanya mkutano na waandishi wa habari wa Tanzania tuliokuwa pale. Nakumbuka alipomaliza mkutano, nilikwenda kumshika mkono na kumkumbatia, nikamueleza kwamba nimefurahi kwa kilichotokea. Bashe alikuwa ametoka kueleza waandishi wa habari kuhusu makubaliano ya Tanzania […]

Prof. Janabi: Jeshi la Mtu Mmoja

Na Ezekiel Kamwaga MAJUZI nilihudhuria harusi moja jijini Dar es Salaam na wakati muda wa kwenda kula ulipofika, MC akatania “wakati tunapokwenda kupakua chakula, msisahau ushauri wa Profesa Janabi”. Ukumbi mzima ulilipuka kwa vicheko. Ni kama kila mtu alikuwa anamjua Profesa Mohamed Janabi na ujumbe wake kwa jamii yake. Kwa hakika, katika mwaka 2023, hakuna […]

Nani atataka kuwa Katibu Mkuu wa CCM?

Picha: Daniel Godfrey Chongolo. Kwa hisani ya tovuti ya CCM.   Na Ezekiel Kamwaga   WIKI mbili zilizopita, mmoja wa rafiki zangu ambaye ni kiongozi serikalini, alikuja Dar es Salaam kikazi. Katika mazungumzo yetu tulipoonana, suala la kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, lilichukua sehemu kubwa ya mazungumzo yetu.   […]

Mafunzo kutoka Zambia

  Na Ezekiel Kamwaga   OKTOBA mwaka huu, nilikuwa sehemu ya waandishi wa habari wa Tanzania waliokuwa kwenye ziara ya kitaifa ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Zambia. Ingawa vyombo vyetu vya habari viliandika kuhusu masuala makubwa yaliyotokea huko, jicho langu lilivutwa na jambo lingine dogo nililoshuhudia.   Oktoba 24, nilipata fursa ya kuhudhuria sherehe […]

Katibu Mkuu wa CCM: Historia Fupi

Na Ezekiel Kamwaga DANIEL Godfrey Chongolo amemaliza muhula wake kama Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuandika barua ya kujiuzulu na kuhitimisha takribani miaka miwili na miezi saba ya kutumikia nafasi hiyo. Wakati alipotangazwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, si watu wengi walikuwa wamewahi kumsikia kabla – ingawa aliwahi kuwa Mkuu wa […]

Maji kila sehemu lakini hakuna maji!

Na Ezekiel Kamwaga   “Maji kila mahali lakini hakuna hata tone moja la kunywa” Samuel Taylor Coleridge, The Rime of the Ancient Mariner   MWANZO kabisa, napenda kutoa pole kwa Watanzania wenzangu ambao wameathirika kwa namna moja au nyingine na mvua hizi za El Nino zinazoendelea kunyesha.   Ninafanya kazi kwenye kituo cha televisheni na […]

Fungulia John Heche Suguta

Picha: John Heche (kwa hisani ya mtandao wa Millard Ayo)   Na Ezekiel Kamwaga   MWAKA 2016 utabaki kuwa na historia ya kipekee kwenye miaka ya karibuni na pengine mingi inayokuja. Huu ndiyo mwaka ambapo neno moja lilitajwa kuwa neno lililotumika zaidi katika lugha za Kijerumani na Kihispania mtawalia; Postfaktisch na Posverdad. Kwenye Kiingereza, linajulikana […]

Bahati na kupanda kwa Dk. Tulia Ackson

Picha: Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) akizungumza baada ya kupokewa katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma mara baada ya kurejea nchini akitokea nchini Angola alikoshinda uchaguzi wa taasisi hiyo ya mabunge duniani. Picha kwa hisani ya mtandao wa Zanzinews.   Na Ezekiel Kamwaga   WAKATI Ikulu ilipotoa […]